Tuesday 12 December 2017

Namna ya Kuboresha ufugaji wa Kuku

Wafugaji wengi wa Tanzania wanafuga kuku wa kienyeji. Ndege hawa kwa kawaida wanafugwa sehemu za vijijini ambapo wanaachiwa huru kuzurura.

Kuna uwezekano mkubwa sana wa kizazi kujirudia kwa kuwa jogoo anaweza kumpanda mtetea ambaye alitokana naye, au kumpanda mtetea ambaye wamezaliwa pamoja. Kuzaliana kwa namna hiyo kunasababisha matatizo makubwa, ikiwa ni pamoja na kudumaa, kupunguza uzalishaji wa mayai, kuwa na vifaranga dhaifu ambavyo ni rahisi kushambuliwa na magonjwa, na mengineyo mengi yasiyokuwa ya kawaida. Ufugaji huru ambao una udhibiti ni muhimu sana ili kuepuka kizazi kujirudia. Kuku wanaweza kuwekwa kwenye makundi na kuachiwa kwa makundi ili kuzuia uwezekano wa kuzaliana kwa kizazi kimoja.

Tuesday 21 November 2017

UTAGAJI NA UATAMIAJI WA MAYAI:



a.       Kuku huanza kutaga wakiwa na umri wa majuma 22-32 baada ya kuzaliwa kutegemeana na 
ukoo ,afya na lishe.Kwa kawaida kuku wa kienyeji /asili watachelewa kutaga kuliko wa kisasa . Matetea hufikia kiwango cha juu cha utagaji wakiwa na umri wa wiki 40-50 na baada ya umri huo utagaji huanza kupungua kidogokidogo. Hali hiyo inapoanza kujitokeza wafugaji wanashauriwa kuuza au kuchinja kuku waliofikia umri huo.